Emmanuel Mbasha kujibu tuhuma dhidi yake za kumbaka shemeji yake
Emmanuel Mbasha, ambaye ni mume wa mwimbaji nguli wa nyimbo za
Injili, Flora Mbasha amejitokeza hadharani na kusema kwamba atakwenda
polisi mwenyewe kujibu tuhuma dhidi yake za kumbaka shemeji yake mwenye
umri wa miaka 17
Faili la tuhuma dhidi ya
Mbasha lilifunguliwa Jumatatu iliyopita katika Kituo cha Polisi Tabata
(Tabata Shule) wakati shemejiye huyo (jina tunalihifadhi), alipotaarifu
kuwa Mbasha alimbaka mara tatu kwa siku mbili tofauti. Kesi hiyo ilipewa
namba TBT/RB/3191/2014 na TBT/IR/1865/2014.
Maoni
Chapisha Maoni