MAONI NA USHAURI WA NASH MC ZUZU KWA MATAMASHA YA KILIMANJARO TOUR NA FIESTA
Miaka
mingi sasa hakuna kitu kipya katika mfumo mzima wa show zenu hasa pale
wasanii wanapokuja kutumbuiza,mashabiki hua tunajua tu kua msanii
atapanda peke yake au siku hizi na wacheza show wake na ataimba kwa
kufuatisha cd yake (PLAYBACK) kwa sehemu ndogo tu ya wimbo wake kisha
baadae watacheza show na atashuka na kama ni wa kike
atadili na suala la kukata viuno wanaume wamshangilie,kwa kweli
mnawadumaza wasanii na suala la wao kwenda kimataifa silioni,angalieni
utaratibu wa kuweka wasanii wachache na watakaokua na uwezo wa kupiga na
Band au waambieni waache kuimba kwa kufuatisha cd zao (PLAYBACK) kwani
inaonesha wazi hakuna ubunifu wala hamzingatii taratibu za
muziki,msiangalie kutangaza biashara zenu au kuuza vinywaji vyenu pia
muhusike ktk kuboresha na kuongeza ufanisi ktk kazi za sanaa,hasa muziki
ambao mmejikita kutangazia kampuni zenu,kila napokaa kwenye tv nitazame
wasanii wenzangu wanachofanya ktk show pengine ntajifunza kitu matokeo
yake nazima na sipati chochote!
Haya ni maoni na ushauri wangu.
Haya ni maoni na ushauri wangu.
Maoni
Chapisha Maoni