Hatuna haja ya kufichana tiba ni kuweka wazi,ukimwi ni upungufu wa kinga elimu kwa hiki kizazi,kuelimisha tukishindwa nani aokoe jahazi
Baada
ya Juma kujua ni muathirika kulimuathiri kifkra siku moja akazidiwa
akaona aiage familia,zikamjia hisia,akaamua kujisalia,akajiinamia huku
Mungu akimlilia,kwa uchungu akamwambia,bado naipenda Dunia,akaanza
kuomba-Nakushukuru kwa uhai,nitakufuru nikikudai,ingawa ninaumwa nina
uhuru usiotozwa ushuru sishangai,kunidhuru haujawahi,umeninusuru tokea
niko yai,uzima ni zaidi ya lulu dhambi zinaongezeka
duniani hatujai,Mola mimi nateseka ukinilinda nitajidai,sikuchagua
kupinda kuharibika hakufai,majaribu nimeyashinda shingo inakufa na
tai,yote umeniwezesha ww ni muweza sikatai,ulimwengu unapendeza naomba
uzima nifurahi,matumaini nitaendeleza niishi nitoe rai,sitorudia kucheza
sitokunywa divai,akatia nia na imani, alikula si utani,matonge hayaishi
kinywani,hana budi kuwa sawa,akawa anameza dawa,mwili ukarudi
kibonge,siri juhudi asikonde,hakuitamani pombe,hata raia
wachonge,asikonde asonge,uzani wa vidonge,mitihani ikampa donge,hakuna
bingwa wa maradhi,hatuna haja ya kufichana tiba ni kuweka wazi,ukimwi ni
upungufu wa kinga elimu kwa hiki kizazi,kuelimisha tukishindwa nani
aokoe jahazi,wanaombukizwa sio wajinga waambieni watoto wazazi,muda wenu
tumieni sio ukuda fundisheni haitoshi shuleni nyumbani wekeni
jamvi,Juma bado anaishi afya njema sasa ni ustadhi,ametulia vyema anasa
kwake haina hadhi,na huwa hasiti kuusema mkasa wake kwa baadhi.
Salu Tee
Salu Tee
Maoni
Chapisha Maoni