Mwimbaji maarufu nchini Ghana Castro anaripotiwa kufa baada ya kujaribu kumuokoa msichana mmoja aliyeanguka ndani ya maji.
Polisi nchini Ghana wanatafuta mwili wa mwimbaji maarufu anayehofiwa
kufa maji baada ya kupata ajali ndani ya maji. Msanii huyo, Castro wa
miondoko ya Afrobeats anaripotiwa kufa baada ya kujaribu kumuokoa
msichana mmoja aliyeanguka ndani ya maji karibu na hoteli moja iliyopo
karibu na baharini. Chombo alichokuwa akiendesha (Jet ski) kimepatikana
na polisi. Castro ambaye jina lake halisini ni Theophilus Tagoe alikuwa
amerejea Ghana wiki iliyopita na alikuwa wakiburudika na nahodha wa
Black Stars Asamoah Gyan, mabaye ni rafiki yake wa karibu.
Maoni
Chapisha Maoni